Kila jambo lino mambo yake katika maisha. Kuna mambo ya kusimamia maneno ya dunia, tena kuna mambo ya kusimamia maneno ya roho na ya kushirikiana na Mungu.


1. MUNGU MWENYEWE ANAKUPENDA, ANATAKA KUKULETEA TARATIBU ZURI KWA MAISHA YAKO.

MAPENDO YA MUNGU
Kwa maana Mungu alivyopenda ulimwengu, hata kutoa Mwana wake wa pekee, ili kila mutu akimwamini asipotee; lakini apate uzima wa milele. (Yoane 3:16).

TARATIBU YA MUNGU KWAKO
Mimi nilikuja ili wapate uzima, na waupate tele. (Yoane 10:10)

Kwa sababu gani watu wingi hawana ushirika na Mungu?
Ni kwa sababu....


2. MWANADAMU Nl MWENYE ZAMBI, NA ZAMBI ZINAMUTENGA MBALI NA MUNGU.
Hivi hawezi kujua mapendo ya Mungu na kushirikiana naye.

MWANADAMU NI MWENYE ZAMBI

Kwa sababu wote wamefanya zambi, na kupungukiwa na utukufu wa Mungu.Waroma 3:23

Mungu aliumba watu, kusudi washirikiane naye. Lakini watu wakapita pembeni ya mapenzi yake, wakachagua kuasi kuliko kutii. {Kuasi Mungu ni zambi). Mutu anapoishi bila mapenzi ya Mungu, anaendelea kufanva zambi.

MWANADAMU AMETENGWA NA MUNGU

Lakini maovu yenu yamewatenga na Mungu wenu. Isaya 59:2

Zaire1

Mungu Mutakatifu hana ushirika na zambi. Kati yake na watu kuna shimo kubwa, na shimo hili na zambi za watu. Watu wanajaribu njia nyingi kwa kutafuta kuvuka shimo kufika kwa Mungu. Wanapima: dini, matendo mazuri, kutoa sadaka na vivi hivi. Lakini wanashindwa kufika kwa Mungu sababu wangali na zambi.

Kuna njia moja tu ya kupatana na Mungu ...


3. YESU KRISTO PEKEE NDIYE NJIA YA KUONDOSHA ZAMBI. Alijitoa kuwa zabihu, ili tuweze kushirikiana na Mungu na kujua taratibu yake kwetu.

ALIKUFA NA ALIFUFUKA TOKA WAFU

Kwa maana Kristo naye aliteswa mara moja kwa ajili ya zambi, mwenye haki kwa ajili ya wasio haki, ili atulete kwa Mungu. 1 Petro 3:18

Kristo alikufa kwa ajili ya zambi zetu kama maandiko yanavyosema; na ya kama aiizikwa, akafufuka siku ya tatu, kama maandiko yanavyosema. Wakorinto 15:34

YESU PEKEE NDIYE NJIA

Yesu akamwambia: Mimi ndimi njia, na kweli, na uzima: mutu hakuji kwa baba, ila kwa mimi. Yoane 14:6

Zaire2

Watu hawangeweza kujifikisha kwa Mungu. Mungu alikuja katika dunia ndani ya Mwana wake Yesu, alizaliwa mutu, akakufa musalabani, ili musalaba uwe kilalo kwa kutufikisha kwa Mungu.

Sasa Jambo la ine inakuambia namuna unavyoweza kujua Mungu na kushirikiana naye katika maisha yako.


4. SHARTI KILA MUTU APOKEE YESU KUWA MWOKOZI NA BWANA YAKE. Hivi tutaweza kujua mapendo na taratibu ya Mungu katika maisha yetu.

 

TUNAPOKEA KRISTO KWA NJIA YA IMANI

Lakini wote waliomupokea, aliwapa uwezo wa kuwa watoto wa Mungu. Ndio wale walioamini jina lake. Yoane 1:12

Kwa maana mumeokolewa kwa neema, kwa njia ya imani, wala neno hili halikutoka ndani yenu wenyewe, ni zawadi ya Mungu. Si kwa matendo, asiwe mutu atakayejisiful. Waefeso 2:8,9

KUPOKEA KRISTO Nl KUMUKARIBISHA KATIKA MAISHA YETU

Kristo anasema: Tazama, ninasimama kwa mulango,ninapiga hodi; kama mutu akisikia sauti yangu na kufungua mulango, nitaingia kwake, Ufunuo 3:20

Maelezo yanayofuata yanakuonyesha namuna unavyoweza kupokea Kristo.

Zaire3


UNAWEZA KUOMBA KRISTO SASA KUINGIA KATIKA MAISHA YAKO.

Mungu anajua moyo wako, na anajua mahitaji yako. Wakati unapomuomba umuombe kwa roho ya kweli, kuomba kwako kusiwe kwa midomo tu. Sasa maneno hayo yanaweza kukusaidia kwa kuomba.

Bwana Yesu, ninakuhitaji. Zambui zangu zimenitenga mbali nawe. Ninakushukuru kwa ahadi yako kwamba utanisamehe zambi zangu zote. Sasa ninakuomba, uingie katika maisha yangu, unitawale. Uongoze maisha yangu kama unavyopenda.
Amina

Maombi haya yanaonesha ile ungependa kusema?

Kama ni hivi, uombe sasa, na Kristo ataingia moyoni mwako.


NAMUNA YA KUJUA KAMA KRISTO YUKO KATIKA MAISHA YAKO

Umepokea Kristo sasa katika maisha yako7 Mungu ameahidi kwamba Kristo ataingia moyoni mwako.
Unazani si kweli? Ahadi ya Mungu inahakikisha neno hili.

BIBLIA INASEMA: UZIMA WA MILELE Nl KWA WOTE WANAOPOKEA KRISTO KWA IMANI

Na hau ndiyo ushuhuda, ya kwamba Mungu alitupa uzima wa milele; na uzima huu ni katika Mwana wake. Yeye aliye na Mwana ni mwenye uzima, lakini yeye asiye na Mwana wa Mungu hana uzima. Ninawaandikia ninyi wenye koumini jina la Mwana wa Mungu maneno haya, ili mujue ya kuwa muna uzima wa milele. 1 Yoane 5:11-13

Shukuru Mungu kwani Kristo anaishi pamoia nawe. Uamini kwamba Yesu hatakuacha kabisa. (Waebrania 13:5). Umepata uzima mupya katika Kristo kama alivyoahidi.


USITEGEMEE MAFIKILI YAKO KWA KUKUONGOZA

Siku nyingine utafurahi kwa mafikili yako, siku nyingine utakuwa na huzuni ao shaka, Si neno. MuKristo wa kweli anasimama na imani, akitegemea Mungu na ahadi zake katika Biblia. Anajua kwamba Mungu ni Mwaminifu, na neno lake ni la kweli. Picha hii ya gari na remorque yake inaonyesha maneno matatu.

  1. UKWELI: maana yake- Mungu na neno lake.
  2. IMANI: maana yake - kutii na kutumaini
  3. MAFIKILI: masna yake - Mawazo ya ndani.

Zaire4

  1. Moteur inaongoza camion. Hivi, ukweli ya Mungu unahitaii kuongaza muKristo.
  2. Essence inaacha moteur kutumika. Hivi imani ni kutuata na kutumaini ukweli ya neno la Mungu.
  3. Remorque inakokotwa nyuma. Hivi, mafikili inakokotwa nyuma, hayawezi kutuongoza.
  4. Sisi tunategemea Mungu na ukweli wake, hapana mafikili yetu.

KWA KUWA SASA UMEPOKEA YESU

Wakati ulipopokea Yesu, ilitokea mabadilliko mengi.

  1. Kristo aliingia katika maisha, yaio (Ufunuo 3:20 na Wakolosia 1:27
  2. Umesamehewa zambi zako. (Wakolosia 1:14)
  3. Umekuwa mwana wa Mungu. Yoane 1:12)
  4. Utaendelea kujua mapenzi ya Munga na taratibu yake katika maisha yako. (Yoane 10:10 na 2 Wakorinto 5:14, 15, 17)

Unafikili kuna jambo zuri kuliko kupokea Yesu? Hapana.

Ungeweza kushukuru Mungu kwa rehema yake kwako?

Tunaonesha imani yetu kwa Mungu wakati tunapomushukuru kwa maambi. . . Hivi tuombe.

Utafanya nini sasa?


NAMUNA MUKRISTO ANAVYOWEZA KUPATA NGUVU KATIKA ROHO

...Mwenye haki ataishi kwa imani Wagalatia 3:11
Imani itatuwezesha kukua na kuendelea kila siku.

  1. Zungumuza na Munga kwa maombi kila mara. Yoane 15:7
  2. Soma Biblia kila siku. Matendo ya Mitume 17:11 Inafaa kuanzia katika Habari Njema ya Yoane
  3. Uwe mwaminifu kwa Munga na kumutii. Yoane 14:21
  4. Ushuhudie Kristo katika maisha yako na katika masemo yako. Matayo 4:19 na Yoane 15:8
  5. Utegemee Munga kwa kila jambo maishani mwako. 1 Petro 5:7
  6. Uitlke Roho Mutakatifu kukutawala na kukuwezesha katika maisha yako ya kila siku, hata uweze kushuhudia Kristo mbele ya watu.

NI SHARTI WAKRISTO KUSHIRIKIANA

Biblia inatuambia: tukusanyike na kushirikiana pamaja. Waebrania 10:25

Wakati kuni zinawekwa pamoja, zinawake vizuri. Lakini tukiweka kuni moja pembeni, pekee yake itaanz kuzimika. Ndivyo ni vigumu kwa muKristo kufuata Mungu vizuri bila kushirikiana na waKristo wengine.

Hivi sharti ushirikiane na waKristo wenzako waliopokea Yesu kama Mwokozi wao.

Uhuzurie kanisa lenye kuhubiri Neno la Mungu la kutii Bwana Yesu.

KAMA KITABU HIIKI KIMEKUSAIDIA, UKILETE KWA MUTU MWINGINE AO UMUSOMEE'


ADDITIONAL ASSISTANCE